Haki za binadamu nchini Tanzania

Haki za binadamu nchini Tanzania haziheshimiwi kiasi cha kuridhisha. Kwenye ripoti "Uhuru katika Ulimwengu ya mwaka 2013, Freedom House iliainisha kuwa nchi hiyo ni "Huru kwa sehemu". [1]

Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mnamo Oktoba 2011 katika mkutano wake huko Geneva lilikamilisha Mapitio ya Ulimwenguni (UPR) ya hali ya haki za binadamu nchini Tanzania. Katika Pitio hilo, Timu ya Umoja wa Mataifa (UNCT) na nchi kadhaa zilishughulikia matatizo mbalimbali nchini Tanzania.

  1. Freedom in the World 2013

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy